• +255 683 865 660
  • This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
  • Mon-Fr 8:00 Am - 15:30 Pm
div class="sp-layer" data-position="topLeft" data-horizontal="50" data-vertical="100" data-show-transition="left" data-show-duration="500" data-show-delay="100"> Sample html content goes here...

About Us

About Us

Image

About Hazina Saccos Ltd


HAZINA SACCOS ni nini?
Ni Ushirika wa Akiba na Mikopo kwa ajili ya kuinua, kustawisha na kuboresha hali za wanachama wake.

Historia
Ushirika huu ulianzishwa mwaka 1972 na kusajiliwa rasmi tarehe 21/03/1973 na wanachama wasiopungua 250.

Dira(vision):
Ni kuwezesha na kuboresha Ushirika wa Akiba na Mikopo ambao utatoa huduma za kifedha ili kukidhi matarajio ya wanachama.

Dhamira
kuwa na ushirika wa fedha wenye nguvu kwa kukidhi mahitaji ya wnachama kwa huduma na mazao.

KWA NINI UJIUNGE HAZINA SACCOS?
HAZINA Saccos ndio chama pekee Tanzania kinachohudumia watumishi wa Umma Serikali kuu, Serikali za mitaa na mashirika yake Tanzania bara.

  • HAZINA Saccos ni chama imara ambacho kimekaguliwa na shirika la ukaguzi (COASCO) na kupata hati inayoridhisha kwa miaka mitanno mfululizo.
  • HAZINA Saccos hutoa huduma bora kwa wakati kama:
  • Mikopo ya Dharula
  • Mikopo ya kulipia ada kwa mwanachama, mtoto au tegemezi yeyote anayemuhusu mwanachama.
  • Mikopo ya kufanyia maendeleo ya Biashara au Ujenzi.
  • Kukopa kwaajili ya huduma za misiba kwa wale wanaowahusu wanachama wa hazina saccos.
  • Mikopo ya viwanja.
  • Inalipa riba kwenye akiba za wanachama.
  • Inatoa gawio kwa wanachama baada ya kupitishwa kwa mkutano mkuu.
  • Inatoa elimu ya ushirika kwa wanachama wake

Lengo kuu (General Objective)
Ni kukuza ushirika wenye uwezo wa kujiendesha kwa kulipa gharama zake kukidhi mahitaji ya huduma ya kifedha ya wanachama bila kutegemea asasi/mamlaka/ watu wengine na kutoa msukumo wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii na kuwa sehemu ya mtandao wa huduma za kifedha katika misingi, njia na taratibu za Ushirika.

Malengo Mahsusi (Specific Obejectives):

·         Kuweza kukuza na kuendeleza huduma endelevu za kifedha kushiriki na kuhamasisha na kuhimiza uwekezaji wa Akiba, utunzaji salama na uhakika wa Akiba na Hisa.
·         Kuweza kujiendelesha kwa faida ili kujiimarisha na hatimaye kujitegemea kifedha na kujitosheleza kiuchumi.
·         Kuweza kutoa bidhaa mbalimbali za mikopo zifaazo kwa wanachama.
·         Kuweza kutoa Elimu ya UJASILIAMALI kwa wanachama.